Your Health Is Our Priority

Your Health Is Our Priority

Fahamu umuhimu wa vyakula mbalimbali

Jua vyakula na mimea tiba maalumu kwa ajili ya afya bora kwako na kwa familia yako

Dondoo za ndoa Bora na yenye Furaha

Fahamu jinsi ya kuimarisha na kuijenga Ndoa yako iwe imara na ya mda mrefu

Dondoo za Mazoezi yatakayo kukinga na Magonjwa mbalimbali

Fahamu mazoezi bora na yenye manufaa yatakayo kuweka vizuri na kukinga na Magonjwa Mbalimbali

Dondoo za Malezi Bora ya Mtoto

Fahamu saikolojia ya watoto,malezi bora na vitu wavitakavyo kwa ajili ya ukuaji mzuri na furaha

Fahamu MbogaMboga na matunda ambayo ni muhimu sana kwa afya yako

Pata taarifa juu ya mbogamboga na matunda,misimu yake pamoja na faida zake

Friday, August 12, 2016

Kutizama Tv kunaweza kukuua, utafiti

Utafiti uliofanywa na wanasayansi wa Japan umethibitisha kwamba kukaa kwa mda mrefu na kutazama vipindi vya televisheni kwa masaa mengi kunahatarisha afya kwani huhusishwa na maradhi yanasababisha mzunguko wa damu mwilini kutokuwa sawa.
Watafiti hao wanasema, hali hiyo pia huenda ikasababisha damu kuganda na kutengeneza vidonge katika sehemu kama vile miguu, na iwapo mgando huo utasukumwa na nguvu za mzunguko wa damu na kuingia sehemu kama vile mapafu, husababisha vifo.
Utafiti huo ulihusiha watu zaidi ya 86,000 ambao hupendelea kutazama televisheni katika mida mbalimbali kwa siku.
Kisha afya zao zilifuatiliwa kwa zaidi ya miaka 19 tangu mwaka 1988 hadi 1990.
Matokeo yalikuwa kila muda wa masaa mawili yalipopita mtu akikaa kutazama televisheni, nayo hatari ya kupata ugonjwa huo wa mapafu uitwao ‘Fatal pulmonary embolism’ ulioongezeka kwa asilimia 40%.

Iligundulika pia kuwa waliotazama vipindi vya televisheni kwa zaidi ya saa 5 walikuwa katika hatari zaidi kuliko waliotazama televisheni kwa mda wa chini ya saa 3.
Zaidi ya hayo watu huambatanisha kitendo cha kukaa na kutazama televisheni huku wakila vitafunio kama vile Popcorns na Crisps ambavyo pia huwasababishia si tu mwili kukosa mazoezi bali pia kuongezeka kwa uzito unaohatarisha afya.

Monday, April 25, 2016

Atumia vidonge vya nguvu za kiume kuzoa kura

Katika mataifa mengi ya Afrika wakati wa uchaguzi wanasiasa hutoa pesa ilikuwashawishi wapigaji kura kuwachagua.
Lakini huko Korea Kusini amini usiamini, polisi wameanzisha uchunguzi baada ya kuibuka madai kuwa wapiga kura wenye umri wa makamo walimpigia mwanasiasa fulani eti kwa sababu aliwapa vidonge vya kuongeza nguvu za kiume!
Yamkini mwanasiasa mmoja aliwashawishi watu hao wenye umri wa makaomo kwa kuwapa vidonge.
Mbunge wa eneo hilo la Suwon iliyoko karibu na mji mkuu wa Seoul ndiye anayetuhumiwa kwa njama hiyo.
Suwon ilishuhudia upinzani mkali katika uchaguzi uliofanyika Jumatano iliyopita
jina la mshukiwa mkuu halijatajwa hadi ushahidi utakapopatikana.Hata hivyo uchunguzi wa msingi umethibitisha kuwa mgombea huyo alikuwa na kiwango kikubwa mno cha madawa ya kuongeza nguvu za kiume kwa wakati mmoja.
Haijabainika ni kwanini wala alikusudia kuwapa kina nani.
Uchunguzi bado unaendelea.