Your Health Is Our Priority

Your Health Is Our Priority

Sunday, October 18, 2015

Faida 5 Kubwa Za Machungwa

1.Machungwa hupunguza Shinikizo la damu.
Virutubisho (Phytonutrients) vitwavyo herperidin’s vipatikanavyo katika machungwa  vinasaidia kupunguza shinikizo la damu.Pia tunda hili jamii ya citrus lina kiasi kikubwa cha folate ambayo husaidia kupunguza uwezekano wa kupata cardiovascular deseases(Magonjwa  ya moyo).



2.Hupunguza Lehemu(Cholestrol) kwa kiasi kikubwa.
Limonin ambayo hupatikana katika machungwa husaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza cholestrol katika mwili wa binaadamu.

3.Huzuia Magonjwa ya Figo.
Machungwa husaidia kuzuia mawe katika figo(Kidney Stones) na husaidia figo kuchuja sumu ziingiazo mwilini ipasavyo.Kunywa 1/2 mpaka  Lita 1 ya juisi ya machungwa kwa siku itasaidia kupunguza kiasi cha pH  katika mkojo kitu ambacho kitapunguza uwezekano wa kutengenezwa mawe(Kidney stones) katika figo.

4.Hupunguza uwezekano wa kupata Ulcers(Vidonda vya tumbo)
Je umechoka kupata Ulcers?au unataka usipate? Basi tunda la chungwa ndio mkombozi wako.Kiasi kikubwa cha vitamin C kipatikanacho katika chungwa kinasaidia kuulinda mwili kutokana na Helicobacter pylori(H.pylori) bacteria ambae husababisha peptic Ulcers(Vidonda  vya tumbo).Vidonda  vya tumbo vikijirudia mara kwa mara humsababishia mgonjwa kupata kansa ya tumbo baadae katika maisha hivyo jilinde kwa kuhakikisha unakunywa japo glasi moja tu ya juisi ya machungwa kwa siku.

5.Kinga ya Mwili(Immune Support)
Tunda la chungwa lina kiasi kikubwa cha vitamin C ambayo huukinga  mwili kutokana na bacteria na virusi.Vitamin C ni muhimu kwa kusaidia kuharibika kwa celi (preventing cell damage) kwa kuondoa free radicals na kulinda DNA (Cancer prevention).Pia VitaminC inasaidia mfumo wa kinga ya mwili na husaidia kuzuia mafua na infections katika  masikio.



1 comments:

  1. Machungwa yana faida nyingi sana na nyingine bado wataalamu wanazifanyia utafiti

    ReplyDelete